Posts

Image
 Simulizi: JIRANI KAMA JIRANI! Imeandikwa na: Abyas Mzigua  Sehemu ya pili ILIPOISHIA:  Mke wangu aliondoka nyumbani. Akaniacha mwenyewe. Mchana jirani yangu akaja na kuniletea chakula, pamoja na kujitahidi kukikataa kwa kumueleza nimekwisha kushiba, bado alinilazimisha na kuniambia nikihifadhi nitakula usiku. Hapo sikuweza kumpinga.  Sasa tuendelee!   Kama ambavyo niliwaeleza, lile poti la chakula nililipokea na kuliingiza ndani. Nikaliweka mezani na kurejea kwenye usingizi wangu. Nilikuja kushtuka kagiza kanakaribia kuingia. Nikagundua kuwa usingizi wangu ulikuwa ni mrefu sana. Ni kweli nilichoka, mno. Usiku wa jana yake sikuwa nimepata usingizi wa kutosha. Nilikuwa ninafanya kazi ya kumbembeleza mwanamke ambaye hakuwa tayari kunisikiliza.          Chipsi sio chakula kabisa jamani! Yani niliamka njaa imenibana mno. Tumbo jeupeee, linadai chakula tu. Moja kwa moja nikaenda katika meza. Nikalifungua lile poti. Ambalo tangu nilivyolipokea...
Image
  Simulizi: JIRANI KAMA JIRANI! Imeandikwa na : Abyas Mzigua  Sehemu ya kwanza    Hapa tunapoishi ni sehemu yetu ya kwanza tangu tufunge ndoa mimi na mke wangu. Tupo inatimu miaka mitatu sasa. Kiukweli sifikirii kuhama kabisa kwa sababu mama mwenye nyumba ni 'mzungu' vibaya mno.    Kwanza haishi hapa. Hakai kabisa eneo hili. Halafu ukifika muda wa kodi, anaweza akakuachia mwezi mzima wa kujipanga ikiwa tarehe imeshagonga na huna hela ya kumlipa. Sidhani kama kuna pepo nyingine mpangaji angetamani kuipata hapa duniani zaidi ya hii! Sidhani!     Lakini, pamoja na yote hayo, kipo kitu kimoja kinachonipa wakati mgumu mno. Na labda nianzie mbali kidogo ili muweze kunielewa vizuri...        Nyumba zetu hapa zipo tatu. Nyumba tatu kwenye uzio mmoja. Yani kiufupi tupo wapangaji watatu.    Ukiacha mimi na mke wangu, nyumba nyingine anaishi jamaa ambaye yeye kuonekana ni mwezi baada ya mwezi. Sijui ni mtu mwenye kazi gani maana...